Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Wednesday, October 22, 2014

NMB YAWAPA SOMO WATEJA WAKE MBEYA.

Mwenyekiti wa Umoja wa Wateja wa Nmb, Jeremia Mahenge akifungua mkutano wa umoja wa wateja wa NMB katika ukumbi wa RC Mwanelwa

Meneja Mahusiano wa NMB Makao makuu, Dickson Pangamawe, akiwapa somo wateja wake 

Mtaalamu wa Biashara ya kimataifa wa NMB makao makuu Alatunoze Sanga akitoa somo kwa wateja wa Nmb katika mkutano huo

Wateja wa NMB Mkoa wa Mbeya wakiwa makini kusikiliza somo

Afisa mikopo NMB Mbalizi Road HANCESON Kyambi akieleze sasa wanatoa mikopo ya bajaji na pikipiki kwa vijana

Wateja wa NMB makini kuwasikiliza wawezeshaji

Alex Masawe mwezeshaji toka NMB






Mkuu wa Wilaya ya Ileje, Rosemary Senyamule akiongea na mwandishi wa habari

Picha yapamoja


BENKI ya NMB imefanya mkutano wake wa mwaka na umoja wa wateja wao(NMB BUSINESS CLUB) na kuwafundisha ujasiliamali na fursa za biashara.

Katika mkutano huo Wateja hao pia walitoa maoni mbali mbali ya uboreshaji wa huduma za kibenki ikiwa ni pamoja na maofisa wa benki hiyo kutambulisha bidhaa na huduma mpya kwa wateja.

Mwezeshaji katika Mkutano huo alikuwa ni Mkuu wa Wilaya ya Ileje, Rosemary Senyamule, ambaye pia ni Mtaalamu wa Biashara na Ujasiliamali ambaye aliwafundisha wateja hao upatikanaji wa fursa na namna ya kutafuta masoko kwa wakati huu.

Senyamule  pia alitoa wito kwa Wafanyabiashara na Wajasiliamali  kutumia mitandao ya kijamii kutangaza bidhaa zao ikiwa ni pamoja na kutafuta masoko ya kimataifa.

Alisema wafanyabiashara wa sasa hawapaswi kubweteka kwenye maduka yao kusubiri wateja bali wanapaswa kuzunguka kutafuta fursa zingine na kuzitumia ili kujiongezea vipato zaidi na sio kulizika na aina moja ya shughuli anazofanya.

Alisema mitandao ya kijamii ikitumika vizuri kwa wafanyabiashara itasaidia kumtafutia masoko kimataifa na kuitangaza biashara yake kwa gharama ndogo na sio kuwaachia vijana kwamba ndio wanaostahili kutumia mitandao hiyo.

Aliongeza kuwa Tanzania na Mkoa wa Mbeya kuna fursa nyingi ambazo wafanyabiashara wanaweza kuzitumia na hatimaye wakaongeza vipato vyao ikiwa ni pamoja na sekta ya Uwekezaji ambapo aliwataka wafanyabiashara kutumia fursa hiyo na sio kuwaachia wawekezaji kutoka nje.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Umoja wa Wateja wa Nmb, Jeremia Mahenge,alisema tangu umoja huo uanzishwe changamoto nyingi zimetatuliwa kutokana na Benki hiyo kupokea maoni kutoka kwa wateja wao kupitia umoja huo.

Alizitaja baadhi ya changamoto ambazo zimeboreshwa kuwa ni pamoja na ongezeko la mikopo na kupungua kwa makato kwa wafanyabiashara, kupungua kwa foleni wakati wa kupata huduma pamoja na uboreshaji wa huduma ambapo hadi sasa Benki hiyo imeongeza siku za kufanya kazi.

Naye Meneja Mahusiano wa NMB Makao makuu, Dickson Pangamawe, alisema lengo la kuanzisha umoja huo ni baada ya kuona Benki inashindwa kupata maoni kutoka kwa wateja wao kirahisi pamoja na kutambulisha bidhaa zinazoanzishwa na benki hiyo kwa wateja.

Mwisho.

Na Mbeya yetu



No comments: