Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Thursday, August 27, 2015

DK MAGUFULI ATANGAZA KIAMA CHA WEZI, MAJAMBAZI NA MAFISADI SUMBAWANGA, TUNDUMA ,ILEJE NA MBOZI‏

 Mgombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia CCM, John Pombe Joseph Magufuli akihutubia katika mkutano wa kampeni alipokuwa akijinadi leo kwenye Uwanja wa Shule ya Msingi Tunduma, wilayani Momba, Mkoa wa Songwe. Magufuli aliseama kuwa endapo akishinda urais atahakikisha wanafunzi wa shule za msingi na sekondari Kidato cha Nne wanasoma bila kulipa ada yaani bure. Pia alisema barabara inayoingia mpakani kutoka Mbozi itajengwa njia nne tena kwa kiwango cha lami ili kupunguza msongamano wa magari yanayovuka kwenda Zambia.

Dk. Magufuli amesema kuwa akiingia madarakani atahakikisha wezi, majambazi na mafisadi wanaswekwa gerezani. Pia anataka Jeshi la Polisi lenye nidhamu na lenye uwezo wa kupambana na wahalifu wakiwemo majambazi. PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA;KAMANDA WA MATUKIO BLOG.


 Dk. Magufuli akihutubia huku akishangilia na mwanachama wa CCM aliyeshika kadi ya uanachama katika Kijiji cha Ndalambo wilayani Momba ambapo alisimama kwa muda akitokea Sumbawanga mkoani Rukwa akienda Tunduma wilayani Momba kuhutubia mkutano wa hadhara
 Mjumbe wa Kamati Kuu na Halmashauri Kuu ta Taifa ya CCM, William Lukuvi akielezea wasifu wa Mgombea urais wa Tanzania Dk. John Magufuli katika mkutano uliofanyika katika Kijiji cha Lahela, Sumbawanhga Vijijini
Dk. Magufuli akihutubia katika mkutano wa hadhara katika Kata ya LAHELA, Sumbawanga Vijijini
Wananchi wa Kata ya Lahela wakishangilioa alipokuwa akihutubia Dk. Magufuli ambapo aliahidi mambo mbalimbali likwemo kutatua taizo sugu la upatikanaji wa dawa za hospitalini
Dk. Kinana akisalimiana na wagombea udiwani kupitia CCM katika Kata mbalimbali za Jimbo la Sumbawanga Vijijini.
Msafara wa Mgombea urais wa Tanzania kupitia CCM, Dk Magufuli ukiingia katika Kijiji cha Nzoka wilayani Momba, ukitokea Sumbawanga Vijijini, Mkoa wa Rukwa.
Dk. Magufuli akilakiwa na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya
Ni furaha iliyoje kumuona Dk Magufuli
Baadhi ya wakazi wa Kijiji cha Nzoka wakisikiliza  kwa makini hotuba ya Dk. Magufuli

Dk. Magufuli akimtambulisha mgombea ubunge, Dk. Lucas Siame


Wananchi wa Kijiji cha Lwasha wakimshangilia Dk. Magufuli alipozungumza nao aliposimamishwa na wananchi akitokea Sumbawanga mkoani Rukwa.
Wazee wa Kijiji cha Ndalambo wakienda kwenye mkutano wa kampeni uliokuwa ukihutubiwa na mgombeana mgombea urais kupitia CCM, Dk. Magufuli.
Ni furaha iliyoje kwa wakazi wa Kijiji cha Ndalambo kumona Dk. Magufuli
Wafuasi wa Chadema wakimshangilia mgombea urais wa Tanzania kupitia kwa CCM, John Magufuli alipowasili katika Kijiji cha Ndalambo.
Wananchi wakimshangilia na kuahidi kumpigia kura za ndio, Dk Magufuli
Waendesha Bodaboda wakimlaki Dk Magufuli


Mambo yalivyokuwa kwenye Uwanja wa Shule ya Msingi Tunduma, mkoani Songwe


Wananchi wakiahidi kumpigia kura za ndiyo mjini Tunduma


Wana Boda boda wakimlaki Dk. Magufuli
Wananchi wakiwa na hamu ya kumuona Dk. Magufuli
Wananchi wakimkubali Dk Magufuli
Dk Magufuli akimnadi Mbunge mtarajiwa Janeth Mbene
Dk Magufuli akizungumza na mgombea ubunge Jimbo la Ileje pamoja na madiwani
PICHA ZAIDI BOFYA HAPA>>>

1 comment:

Anonymous said...

wataisoma Number.but ongezeni juhudi kutumia mitandao.whatsapp,kukiwa na moja akiambiwa aforward group lingine zinatembea.facebook.electronics ndo mtindo mzima.big up!!