Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Wednesday, April 27, 2016

MAKALLA ATEMA CHECHE KWA WATUMISHI WA HALMASHAURI WAKIWEMO MADIWANI

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Amos Makalla akifafanua jambo mbele ya waandishi wa habari

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Amos Makalla akiongozana na Mkuu wa Wilaya ya Mbeya na viongozi wa Jiji la Mbeya wakikagua Soko la Kimataifa la Mwanjelwa ambalo halitumiki kutokana na wafanyabiashara kuhofia ukubwa wa kodi

Baadhi ya Wafanyabiashara wakilalamikia Chumba kilichokuwa kimetengwa kwa ajili ya Dampo kudaiwa kupangishwa kwa Mfanyabiashara kinyume na matumizi yaliyokusudiwa

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Amos Makalla sambamba na Mkuu wa Wilaya ya Mbeya wakipita mbele ya Vizimba vya wafanyabiashara wadogo ambavyo pia havitumiki kutokana na kodi kuwa kubwa

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Amos Makalla akikagua Soko la Mwanjelwa

MKUU wa Mkoa wa Mbeya Amos Makalla amewaagiza Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya kuhakikisha wanatimiza wajibu wao kwa kuisimamia Halmashauri ili isonge mbele katika shughuli za maendeleo.
Agizo hilo alilitoa  katika ziara yake ya kujitambulisha alipokuwa akiongeza na madiwani, watumishi wa halmashauri, viongozi wa mila na viongozi wa dini katika mkutano uliofanyika kwenye ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya.
Makalla alisema Madiwani wanayonafasi ya kuisimamia Halmashauri kwa kuhakikisha miradi yote inatekelezwa kama inavyotakiwa, pamoja na kusimamia asilimia kumi za mapato kwenda kwenye mikopo ya vikundi  vya Vijana na akina mama.
“Kazi ya madiwani sio kususia vikao na kudai posho, nyie majukumu yenu ni kuisimamia halmashauri kwa kuhakikisha miradi inatekelezwa na zile asilimia kumi zinatengwa na kuwafikia walengwa, kwanza itakuongezea kura kwenye uchaguzi ujao” alisema Mkuu wa Mkoa.
Makalla alisema Madiwani hawapaswi kupokea posho za vikao kama kikao kitakuwa kimevunjika lengo likiwa ni kubana matumizi na kuokoa fedha kwa ajili ya shughuli za maendeleo.
Aidha aliwanyoshea vidole Watendaji wa Kata na vijiji pamoja na viongozi wote kuanzia ngazi ya kijiji kuhakikisha wanasoma mapato na matumizi kwa wananchi ya fedha walizochangia.
“Wasiosoma mapato na matumizi siku zao zinahesabika, haiwezekani mradi mmoja haujakamilika mnawachangisha wananchi michango mingine hapo lazima kuna ufisadi ambao  mbele yake utasababisha migogoro katika jamii” alisisitiza Makalla.
Mkuu huyo wa Mkoa aliagiza kuwa mwaka wa fedha 2016/2017 ni marufuku mawakala kutumika kukusanya ushuru ndani ya halmashauri bali kazi hiyo inapaswa kufanywa na watumishi wenyewe.
“Ni marufuku mawakala kutumika kukusanya mapato kwanzia mwaka wa fedha ujao kwani wanasababisha kero kwa wananchi pia wao wanapata faida kubwa kuliko halmashauri, watumishi wako wengi wengine wanakaa maofisini bure tu hivyo watakaa kwenye mageti kukusanya ushuru kwa kutumia mashine ya kielekroniki” aliagiza Makalla.
Wakati huo huo Makalla aliagiza Watumishi wote katika Mkoa wa Mbeya kurudi kwenye vituo vyao vya kazi kwa ajili ya kuhakikiwa upya ambapo alitoa kuanzia tarehe 20 hadi 24 Aprili 2016 kuwa muda wa kusafiri na kwamba zoezi litaanza Aprili 25 hadi 29,mwaka huu.
Alisema amelazimika kurudia zoezi la kuhakiki baada ya kubainika kuongezeka kwa watumishi hewa katika Halmashauri ya Jiji na Wilaya ya Mbeya ambapo Halmashauri ya Wilaya imeongezeka kutoka watumishi 9 hadi 13 huku Jiji wakiongezeka kutoka 14 hadi 23.
Alisema ili kufanikisha zoezi hilo ameunda kikosi cha watu 14 ambapo mtumishi atapaswa kuonekana kwa sura akiwa na barua ya kazi, kitambulisho na slipu ya Mshahara wa mwisho wa mwezi.

No comments: